NAFASI ZA KAZI MKAGUZI WA NDANI MSAIDIZI NA HOTELI MENEJA

on 1st November 2023 by elct

NAFASI ZA KAZI

KKKT- Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria

S.L.P 423 Mwanza

Tel/Fax + 255 282 540 674                                                 

Barua pepe: info@elct-elvd.org

Tovuti: www.elct-elvd.org

Taarifa kuhusu DMZV: Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria ni moja kati ya Dayosisi 27 za Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania. DMZV inajumuisha mikoa miwili ya Mwanza na Geita.

DIRA YA DMZV: ‘Kuungana katika Kristo ili ufalme wa Mungu utawale.

DHIMA YA DMZV: Kueneza Injili ya Yesu Kristo kwa maneno na matendo kwa watu wote katika mikoa ya Mwanza, Geita na kwingineko.

Uongozi wa Dayosisi unatangaza nafasi za kazi kama ifuatavyo:

v   NAFASI YA KAZI: Mkaguzi wa Ndani Msaidizi

              IDADI YA NAFASI ZA KAZI: Moja (1)

              MAHALI PA KAZI: Ofisi Kuu KKKT-DMZV

              ATARIPOTI KWA: Mkaguzi wa Ndani DMZV

WAJIBU WA KAZI:

  • Kukagua kwa kina vitabu vya fedha kuanzia ngazi ya sharika, vitengo, vituo,majimbo na ofisi kuu
  • Kutoa ushauri wa kuboresha utunzaji mali za Dayosisi na kuboresha vyanzo vya mapato ya ndani nan je
  • Kufanya ukaguzi wa kushtukiza na wa ratiba wa vituo, majimbo, sharika, miradi nataasisi za dayosisi na kutoa taarifa kwa Mkuu wa Dayosisi
  • Kuhimiza matumizi ya fedha katika Hazina Kuu, vituo, majimbo na sharika zitumike kwa kuzingatia makisio yaliyoidhinishwa ipasavyo
  • Kukagua uandikaji wa vitabu na kumbukumbu za fedha za siku kwa siku kuona kuwa mambo yote yametunzwa kwa usahihi na usalama
  • Kukagua taarifa za vipindi vya miezi mitatu (3) katika sharika, vituo na majimbo
  • Kuhakikisha kuwa fedha taslimu zilizo mkononi mwa mhasibu na zilizo benki zinalingana na zilizooneshwa kwenye vitabu vya kumbukumbu za fedha
  • Kuhakikisha kuwa urari kila mwezi ni saw ana unafannyika
  • Kuhakikisha kuwa mahesabu ya mwisho wa mwaka yametengenezwa na kukamilishwa ipasavyo na kwa wakati unaotakiwakuhudhuria vikao anapohitajika bila kura
  • kufanya kazi zingine zitakazopangwa na msimamzi/mwajiri

SIFA ZA MWOMBAJI:

·         Mkristo Mlutheri na mwenye moyo wa kutumika Katika Kanisa

·         Sifa za ziada kama vile CPA (T), CA, ACCA au sifa nyingine zinazolingana zinazotolewa na NBAA

·         Uzoefu wa kazi usiopungua miaka miwili (2) na kuendelea

·         Ujuzi katika matumizi ya Kompyuta na program za kuhifadhi data

·         Elimu kuhusu taratibu, sheria na kanuni za ukaguzi wa fedha

 

SIFA ZA KIELIMU:

·         Shahada ya kwanza ya uhasibu au usimamizi wa fedha kutoka katika chuo kinachotambuliwa na Serikali

 

v  NAFASI YA KAZI: Meneja wa Hoteli

             IDADI YA NAFASI ZA KAZI: Moja (1)

             MAHALI PA KAZI: Charming Bungalow Hotel- Nyakato

             ATARIPOTI KWA: Mkuu wa Idara ya Mipango na Uwekezaji

WAJIBU WA KAZI:

·         Kusimamia na kuhakikisha usalama wa eneo la kazi

·         Kusimamia wafanyakazi katika Hoteli

·         Kubuni njia mbalimbali za uendeshaji wa hoteli

·         Kusimamia na kudumisha uhusiano mzuri wa wageni na wateja

·         Kusimamia na kufuatilia orodha na mali za hoteli

·         Kuandaa, kusimamia na kutengeneza bajeti za uendeshaji wa kituo

·         Kufanya tathimini za kawaida za uboreshaji wa Huduma ya wateja

·         Kukusanya malipo na kudumisha kumbukumbu za bajeti, fedha na gharama

·         Kuandaa ripoti na taarifa ya kazi ya hoteli kila baada ya miezi mitatu na mwaka

·         Kushughulikia malamiko na maswali ya wateja ili kukuza biashara

·         Kusimamia ufuatiliaji wa taratibu za kisheria za Ncji, Afya, Usalama, mapato na Leseni za Hoteli

·         Kuandaa mpango kazi wa kituo, taarifa ya kazi na taarifa ya mapato na matumizi kwa kila mwezi na kuiwasilisha kwa Mkuu wa Idara ya Mipango na Uwekezaji.

·         Kupanga, kutekeleza na kusimamia shughuli za kila siku za hoteli

·         Kufanya kazi zingine utakazo pangiwa na Msimamizi/Mwajiri

 

SIFA ZA MWOMBAJI:

·         Cheti cha usimamizi wa hoteli (Hotel Management)

·         Uwezo mzuri wa mawasiliano ya kutunza mitandao kama barua pepe, facebook, instagram, twitter na kufanya booking.

·         Uwezo mzuri wa kuhudumia na kuzungumza na wateja kwa ukarimu (good customer care and hospitality)

·         Uzoefu wa kazi angalau mwaka mmoja na kuendelea katika hoteli zinazotambulika

·         Mwenye maadili ya Kikristo

·         Mwenye moyo wa kutumika Kanisani

 

SIFA ZA KIELIMU:

·         Stashahada/shahada ya usimamizi wa biashara au fani zingine

 

v  NAMNA YA KUTUMA MAOMBI:

Waombaji wenye sifa wawasilishe Barua za maombi ya kazi, Wasifu (CV), Vivuli vya Vyeti na Barua ya Utambulisho kutoka kwa kiongozi wa Dini kwa:

 

KATIBU MKUU,

KKKT – DAYOSISI MASHARIKI YA ZIWA VICTORIA

BARUA PEPE: elctelvd84@gmail.com  

TAREHE YA TANGAZO: 01/11/2023

MWISHO WA KUTUMA MAOMBI: 20/11/2023                   SAA: 08:00 Mchana

 

NB: Maombi yawasilishwe kwa njia ya barua pepe tu. Na sio vinginevyo

 

KKKT- DMZV inatoa fursa za ajira kwa watu wote wenye sifa.

Mission Statement

ELVD endeavours to spread the gospel of Jesus Christ, through word and deed, to serve all people in the regions of Mwanza, Geita regions.

UPCOMING EVENTS